Ukurasa wa mbele
Soma barua Yahoo
Soma barua Hotmail

 




TV ya INJILI
Kwenye Internet
-
WWW.GOSPELGTV.COM

Tel. 254722602445 E-mail:
munishi@munishi.com or info@munishi.com

Aibu Yaifunika Tanzania

Serikali ya Mkapa imefanya kosa la kiistoria pale ilipowafukuza waandishi wa habari wa nchi jirani ya Kenya. Waliyataka wenyewe, na yalipokuja sasa wanayakimbia. Baada ya gazeti la "Mwananchi' kuuzwa kwa kampuni ya 'NATION", Wakenya waliwekeza mabilioni ya dola za Kimarekani katika sekta ya habari na utangazaji nchini Tanzania. Kile ambacho hawakukijua, ni kwamba sekta hiyo haijawahi kuwa huru Tanzania. Walipoanza kuandika habari kulingana na taaluma yao, gazeti la 'Mwananchi' lilianza kuchanja mbuga Tanzania, na kuwa moja kati ya magazeti yanayoongoza nchini humo. Serikali ikaliona hilo. Kama kawaida yao kuthibiti habari, walijaribu kulitumia gazeti la 'Mwananchi" liwapigie debe CCM wakati huu wa uchaguzi. Inasemekana wanataaluma hao waliikatalia serikali usoni, jambo lililosababisha kutimuliwa kwao. Mkapa ameithihirishia dunia kile ambacho walikuwa wakikijua tayari. Kwamba Tanzania hakuna uhuru wa kutoa mawazo. Na kwamba utitiri wa vyombo vya habari Tanzania ni kifunga macho ili jumuia ya kimataifa ione kwamba kuna uhuru wa habari, kumbe asilimia 99 ya vyombo hivyo humilikiwa na serikali pamoja na maajenti wake. Inasemekana Mkapa mwenyewe anamiliki zaidi ya magazeti 8 yakiwemo yale ya kidini ambayo hayaachi kuweka picha yake mbele. Anapomaliza urais na kuirudia kazi yake ya uandishi, Mkapa atakumbukwa kama mwanahabari aliyepata madaraka yakamlevya, kisha akaanza kuwatesa wanahabri wenzake.



Umewahi kujiuliza kwa nini mabalozi wa Tanzania nchi za nje karibu wote ni wanajeshi wastaafu? Je Serikali huwatumia kufanya ukachero kwenye nchi hizo? Au hujihusisha na mambo ya kidiplomasia kama yalivyo? Je wanajeshi na wanadiplomasia ni taaluma moja? Kwa nini Serikali zote tangu Nyerere zimekuwa zikifuata desturi hiyo? Je ni mbinu ya kuwatawanya wanajeshi ili wasiweke vichwa pamoja kuitoa serikali dhalimu ya CCM? Hayo na mengine mengi, Mwandishi wetu atayaangalia katika makala haya.

Serikali za awamu tatu Tanzania zimekuwa zikiendeshwa kihuni. Wananchi wanatishwa ili wasitoe maoni yao.Vyombo vya dola Polisi, Usalama wa Taifa, Uhamiaji pamoja na vikosi vya siri vimekuwa vikifanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kwamba CCM inaendelea kubaki madarakani. Mengi hufanywa kwa siri sana, kiasi kwamba ukiwa nje ya Tanzania huwezi kuamini kwamba CCM na Serikali zake wanaendesha mambo kihuni. Pengine nakosa neno sawia na matendo ya CCM. Ukiwaita wahuni haitoshi. Ni wauaji, Tena washirikina wa kiwango cha juu sana. Pia nikiwaita wezi haitoshi kulingana namna wanavyofanya wizi wao. Pengine Majambazi Matapeli litakaribia sifa yao. Je mtu anayekuibia na huna pa kumpeleka anaitwaje? Hao ndio CCM. Kwa sababu ya kuendesha mambo kinguvunguvu, wanajeshi huwa wanawafaa sana. Ndiyo maana katika utawala wa CCM wamekuwa wakitumia wanajeshi kuliko raia.Nyerere alijua kwamba Wanajeshi ni amri. Tena wanajeshi wana nidhamu. Isitoshe Wanajeshi hutii halafu maswali baadaye kama watakuwa hai kuyauliza. Ni sababu hizo na nyingine ndizo zilizomfanya Nyerere kuwatumia wanajeshi katika utawala. Alilazimisha wasomi wote kwanza wapitie mafunzo ya Kijeshi kuwakamua kiburi cha usomi. Mpaka leo kamba alizosuka Nyerere hazijakatwa, kwani awamu zote zimekuwa zikifuata mfumo wa Nyerere aliyeanzisha ujamaa ukashindwa.Nyerere aliwafundisha wanasiasa Tanzania jinsi ya kuiba chakula na kupangusa mdomo. Wanaiba, Wanaua, Wanaharibu nchi kwa sera mbovu, Lakini utashangaa Kimataifa Tanzania inahesabika kama kisiwa cha amani wakati si kweli. Ni mpaka mtu mwenye mawazo huru aingie Tanzania hata kama ni mwezi mmoja, Halafu ajaribu kujieleza kwa Watanzania, Ndipo atakapogundua kwamba Tanzania ni nchi tofauti kuhusiana na haki za kibinadamu. Uaskari askari uko kwa kila mtu. Upeo wa kimawazo unafuata mkondo mmoja. Yaani Tanzania iko Ki-Nyerere Nyerere vile. Wanasiasa Tanzania ni sawa vinyonga. Utawaona wapole kumbe ni wezi wakubwa. Hakuna mtu anaeyajua haya nisemayo kama kampuni ya magazeti ya Nation. Walitapeliwa wakauziwa gazeti lililokuwa la chama na Serikali "Mwananchi" Waliponunua na kuanza kufanya kazi ya uandishi kitaaluma, ndipo walipoanza kuuona upande wa pili wa Serikali. "Mwananchi" lilianzishwa 2000 kuelekea uchaguzi mkuu. CCM walilitumia gazeti hilo kwa propaganda. Wafanyikazi karibu wote walikuwa maofisa usalama wa Taifa. Hatujui kama "NATION" walipoinunua kampuni hiyo wafanyikazi wa zamani walibaki. Kama walibaki, "NATION" watajidanganya kusema magazeti yao Tanzania yatakuwa huru mbali na kuingiliwa na Serikali. Wakijaribu kufanya hivyo, Wataiona nguvu kubwa ya CCM ambayo huwa imejificha. Lakini kama "NATION" na kampuni yao mpya "Mwananchi" wataendelea na ujasiri wao wa kufichua mambo, Basi Tanzania itakuwa siyo sehemu nzuri kufanya hivyo. Ni nchi yangu naijua. Nawajua wanasiasa wa Tanzania wanavyoitumia dola kulinda maslahi yao maovu. Sikushangaa niliposoma kwenye "NATION" kwamba Serikali Tanzania ina mpango wa kuwatimua wanahabari wa Kenya.


Serkali ya Tanzania inaongozwa na wahuni. Usipounga mkono maovu yao, basi watakufanya chochote. Watatumia kila chombo cha dola. Idara ya UHAMIAJI ikiwa mojawapo.
Ni kawaida yao. Wamezoea. Na hawapelekwi kokote. Kinachoniumiza moyo, ni mabilioni ya shilingi za Kenya "NATION walizotapeliwa na Serikali ya Tanzania. Kwamba sasa wanawatimua, Mtu anaweza jiuliza kwa nini waliwauzia kampuni hiyo ya "MANANCHI" ikiwa kuwapa vibali ni vigumu? Hata kama wewe ni Mtanzania usishangae kuitwa mkimbizi kutoka Zambia. Wana habari wa "NATION" wako Tanzania kufanya kazi kulingana na taaluma yao na siyo kuipigia debe CCM. Kama Mkapa alifikiri kwamba "NATION" ni "UHURU" na "MZALENDO" magazeti ya chama, atakiona kilichomnyima kuku kutoa maziwa anyonyeshe vifaranga. Namshukuru Mungu kwamba "NATION" wamejionea wenyewe yale ambayo nimekuwa nikiyalalamikia kwa miaka mingi. Kanda yangu ilipigwa marufuku kwa kusema "CCM aliyoanzisha Nyerere imezeeka, Sijui "MWANANCHI" walisema nini. Lakini Wahuni wa DAR, wameanza fujo zao. Safari hii wameuma kubwa kuliko uwezo wao kutafuna. Pengine wateme. Wakimeza itawakwama kooni.Jipeni moyo "NATION" Mungu ni mkuu kuliko CCM na Mkapa mwanahabari anaewatesa wanahabari.Wengine wanasema pengine ni baada ya gazeti la 'Mwananchi' kuandika makala kumhusu Munishi Rais mtarajiwa Tanzania ndipo gazeti hilo likajipata matatani. Kuna wale wanaosema hiyo siyo sababu kwani gazeti hilo pia liliwahi kuandika kumhusu Komba anayejikomba na CCM. Lakini iwe ilivyokuwa tayari Tanzania imejifunua uchi mbele ya dunia ionekane inavyovikandamiza vyombo vya habari.
Gazeti la "MWANANCHI" Lasema:


Gazeti la "MWANANCHI"
Walichokosea ni kutosema kwamba Munishi nitagombea Urais Tanzania. Nia yangu ya kuwa Rais wa Tanzania bado iko pale pale.Kwamba katiba hairuhusu wagombea binafsi, hiyo hainifanyi nijiunge na chama chochote cha kisiasa ili nitimize masharti ya KATIBA. Kwangu siasa ni uongo, na siwezi kujiunga na uongo niwatoe waongo. Ikiwa CCM hawataibadili Katiba iruhusu wagombea binafsi, basi tutaiasi katiba tuandike yetu. Wakichaguana nasi tutachaguana. Kwa mara ya kwanza Tanzania itakuwa KATIBA ya Injili na serikali ya Injili, Rais wa Injili na Bunge la kiinjili.
Hapo ndipo tunapoelekea. Siyo ajabu kwani tayari tuna nyimbo za GOSPEL kilichokuwa kimebaki ni KATIBA ya Gospel Itakayounda tume ya Gospel ya uchaguzi utakaomchagua Rais wa Gospel atakayeunda Serikali ya Gospel akitumia wabunge wa Gospel. Waislamu wakiona vyema wajiunge na Gospel tutawakaribisha. Wakiona waunde yao ya SHARIA, ni sawa. Pia kwa mara ya kwanza Tanzania itakuwa nchi ya serikali zaidi ya kumi. nayote hayo yatafanyika kwa amani. Kikwazo cha amani Tanzania kitakuwa ni CCM pale watakapokataa mabadiliko, na kungangania madaraka.Kama kawaida yao wataanza kuwalaumu wengine. Lakini wananchi safari hii wameerevuka na wanamjua mbaya wao ni nani.CCM ndiye nyoka anayestahili kupondwa kichwa.


Contact us/ Tuandikie

Full Name
E-mail
Subject
Message
   
   

 

 
| http://munishi.com |