Ukurasa wa mbele
Soma barua Yahoo
Soma barua Hotmail

 




TV ya INJILI
Kwenye Internet
-
WWW.GOSPELGTV.COM

Tel. 254722602445 E-mail:
munishi@munishi.com or info@munishi.com

James Kim Apokonywa mchumba

Baada ya kujitafutia mchumba, walipanga siku ya kufunga pingu za maisha. Kabla ya kujuana kimwili, James alimuona mchumba wake akiwa na mimba. Tofauti na ile ya bikira Maria iliyokuwa kwa uwezo wa roho Mtakatifu, Hii ya mchumba wa James ilikuwa kwa uwezo wa Pastor "MWENYE ROHO MTAKAVITU". Pamoja na jitihada za Pastor huyo kumtaka Kim amuoe msichana huyo, inasemekana kwamba juhudi hizo zimegonga mwamba kwani James Kim amekataa kata kata.Ndoano iliyotumika kumnasa binti huyo ni "Huyo Kim ana nini? Tafuta nyumba Buru Buru na kama unataka sana kumuona huyo Kim wako, basi nitamwajiri awe mlinzi wa usiku kwenye hiyo nyumba" Hayo ndiyo maneno yaliyommaliza nguvu mchumba wa Kim. Na kweli inasadikiwa kwamba msichana huyo amekodishiwa nyumba kwenye mtaa wa Buru Buru mjini Nairobi, Lakini kim ameikataa kazi ya WATCHMAN huko. Mengi zaidi muulize James kim Mwenyewe kwenye simu ya mkononi +254723552655

Kanda Mpya

Mwinjilisti James Kim amechomoa kanda mpya. James aliyekuwa mchezaji hodari wa vyombo katika huduma ya Mchungaji James Maina Nganga. Inasemekana kanda yake hiyo, imeanza kupata umaarufu katika Kanisa la Neno Evangelisim. Muda mfupi baada ya kanda hiyo kutoka, uhusiano wake na Pastor ulianza kuzorota, jambo lililopelekea kusimamishwa huduma mara moja. Kwa sasa hana masoko ya kuiuza kanda yake kwani alitegemea kanisani ambako alihudumu kungekuwa soko la kwanza kabla ya wengine kuijua kanda yake. Akiwa katika Ofisi za Gospel GTV, alituonyesha barua aliyopewa kusitisha huduma yake kanisani hapo.


Inaonekana kuna vita baridi kati ya waimbaji na wachungaji. Wachungaji wakiona huduma za waimbaji zinaaza kushamiri, wanaanza mbinu za kuwamaliza kihuduma. Hatuungi mkono utovu wa nidhamu kati ya baadhi ya waimbaji, Pia sambamba na hilo, Hatuwaungi mkono Wachungaji wenye wivu. Matatizo ya waimbaji mengi wamejiletea wenyewe, Lakini ni kweli kwamba wachungaji nao wanachangia pakubwa kuwadidimiza waimbaji. Katika ukurasa huu kumejaa visa vya waimbaji walioteswa mikononi mwa wachungaji wenye wivu na wengine tabia zao haziambatani kabisa na maandiko matakatifu. Hii imeendelea kujenga ukuta mkubwa kati ya waimbaji na Wachungaji. Hakuna sababu ya Mchungaji kuwasakama Waimbaji kwa sababu tu wametoa kanda ili wajitegemee. Kuna ubaya gani kufanya hivyo? Waimbaji wengi hufanya huduma zao makanisani kwa misingi ya kujitolea na siyo vibaya wakijikwamua kiuchumi wakitumia sanaa yao.Wengi hawalipwi, na kama wanalipwa ni kidogo sana kuwawezesha kumudu mahitaji ya kila siku. Kuwatumia waimbaji halafu uwatupe unapofanikiwa kihuduma, ni sawa na kuwaua. Hiyo haimpendezi Mungu hata kidogo.Mapato ya makanisa mengi huishia mifukoni mwa wachungaji wakati waimbaji huambiwa wamtumikie Mungu. Kwani kuna kosa gani kwa muimbaji kumtumikia Mungu huku akitumia sanaa yake kujilisha na kujivisha? Je Wachungaji wanapotumia vibaya pesa za kanisa kwa anasa, Nani awape barua ya kuachishwa kazi? Wengine hudai kwamba wao wameitwa na Mungu kwa hiyo wana haki ya kutumia pesa za kanisa wapendavyo. Siyo kweli.Kanisa ni washirika pamoja na Pastor. Bila washirika kusingekuwepo na pesa ambazo Wachungaji hujivuna nazo

Redio za Injili na Wanamuziki wa Gospel
.
Mwinjilisti Kim akifikiri kazi imeisha, Alijikuta ndio kibarua kinaanza. Alirauka asubuhi kuanza kuzitembelea Redio Stesheni ili ziweze angaa kucheza nyimbo zake ziweze kujulikana. Hakuyaamini masikio yake pale alipoambiwa wazi kwamba lazima atoe kitu ndipo nyimbo zake ziweze kusikika. Kwa kijana ambaye ameachishwa kazi na kupewa Elfu tano ambazo alilipia nyumba zote, kumwambia atoe pesa ndipo nyimbo zake ziwekwe hewani , ni sawa na kumtuma James Kim maziwa ya kuku na sijui atayapata wapi. Baada ya kutoka KBC ambako walichukua CD yake bila kuahidi wataicheza lini, Kim alienda Redio CITIZEN ambako nao pia walimpokea vizuri na kuichukua CD yake. Lakini alipofika kwenye redio ya Injili BHB ambako alitegemea kukaribishwa vizuri kuliko alikotoka, Huko Biblia husema aliambiwa lazima alipe shilingi elfu mbili ndipo nyimbo zake zichezwe. Alipouliza kama atapewa risiti ya pesa hizo isiwe kwamba anatoa rushwa, Alijibiwa kwamba risiti ataipata. Ilimbidi Kim azunguke mguu na njia ili kuweza kupata Kshs.2000. Mungu alikuwa mwema kwake kwani msamaria mwema aliamua kumsaidia baada ya kuelezewa magumu aliyopitia Kim. Alirudi haraka BHB na kuwalipa, na siku hiyo hiyo walianza kuucheza wimbo wake ambao kila anayeusikia anabarikiwa rohoni. Kweli safari ya WOKOVU ina mengi njiani.
Hapa ni risiti Kim aliyopewa BHB baada ya kukataliwa katakata kwamba nyimbo zake haziwezi kuchezwa bure.

Mwinjilisti James Kimwele.
Mungu akikugusa kumsaidia kijana huyu, Fanya hivyo kwa kutumia simu yake +254723552655 Ni mchezaji mzuri wa gitaa, na karibu nyimbo zote alizowahi kuimba mchungaji Nganga kijana huyu ndiye hucharaza Lead Gitaa au Bass.Pia anajua kucheza piano vizuri sana.

Jiandikishe Hapa
Hata kuishi Amerika ni haki yako

 

 
| http://munishi.com |