

TV ya INJILI Kwenye Internet
-
WWW.GOSPELGTV.COM
Tel.
254722602445 E-mail:
munishi@munishi.com or info@munishi.com
Ajali
ya Kutisha
Moja kati ya ajali mbaya Tanzania
Ilitokea mchana maeneo
ya CHAMAKWEZA katikati ya Mlandizi na Chalinze mkoa wa Pwani nchini
Tanzania Afrika ya mashariki. Ilikuwa ni baada ya basi kugongana na
magari matatu.Watu 17 walipoteza maisha yao, 14 walikufa papo hapo
na wengine walikufa wakiwa njiani kuelekea hospitali. Sita kati ya
waliokufa walikuwa kutoka familia moja. Walikuwa wakisafiri kwenye
gari aina ya LAND CRUISER iliyokuwa imetokea Singida kuelekea
Dar. Hayo ni kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Pwani Bwana
Ally Mbilikila.Watu 24 walijeruhiwa vibaya, jambo linaloashiria kwamba
idadi ya waliopoteza maisha yao katika ajali hiyo kuongeeka. Imetajwa
kama ajali mbaya kuwahi kutokea Tanzania. Ilihusisha magari manne,
likiwemo basi la abiria "JVC." Pia iliarifiwa kwamba watu
wa kwanza kuwasili maeneo ya ajali, walijihusisha na kuwapora majeruhi
pamoja na wale waliopoteza maisha.Walionekana wakiwasachi mifukoni
na kuchukua kila walichokipata. Iwe ni simu za kiunga mbali, au pesa
pamoja na mabegi ya kusafiria, vyote viliishia mikononi mwa wezi hao.
Mmoja kati ya majeruhi alisikika akisema kwamba badala wamsaidie kutoka
katika mabaki ya Basi lililohusika kwenye ajali, wao walikuwa wakimpekua
mifukoni bila ya huruma. Dereva wa Lori alikufa papo hapo na hajatambulikana.
Pia kwenye sakata hilo la ajali , ilikuwepo LAND CRUISER nyingine
inayomilikiwa na wizara ya ujenzi. Kilichosababisha ajali hiyo bado
ni kitendawili. Basi la abiria kugongana na magari matatu hiyo ni
ya aina yake.
"Je Ubinadamu uko wapi? Simu Pesa na
Mabegi ya kusafiria yamekuwa muhimu kuliko maisha ya watu? Aibu kubwa
kwa watanzania waliofanya kitendo hicho."
Watatu waponea chupuchupu
Hawa jamaa watatu wa asili ya kieshia wameponea
chupuchupu baada ya gari lao kukosa njia na kugonga nguzo ya umeme.
Ajali hiyo iliyotokea katika barabara ya Ngong sehemu ya Lenana asubuhi
ya tarehe 2/.7/2005. Abiria wawili pamoja na dereva walifanikiwa kutoka
bila majeraha yeyote, lakini gari lao liliungua nyanga nyanga. Tofauti
na vibaka wa Tanzania waliowapora majeruhi, Wakenya waliofika sehemu
ya ajali walionekana kuwasaidia waeshia ambao walikuwa na kiwewe pamoja
na kuchanganyikiwa.
45 walipuliwa London
Watu 45 wameripotiwa kufa huku wengine 700 wakijeruhiwa vibaya mjini
London baada mabomu kulipuka sehemu mbali mbali nchini Uingereza Alhamisi
ya tarehe 7/7/2005. Kundi la Alkhaida linaloongozwa na Osama Bin Laden
limedai kuhusika na milipuko hiyo, Katika taarifa waliyoitoa kupitia
Mtandao wa kompyuta duniani. Taarifa hiyo ilisema kwamba wamelazimika
kulipua London ili kulipiza kisasi mauaji ya maelfu ya raia wa Irak
yanayotekelezwa na majeshi ya uingereza, ambayo kwa sasa yako nchini
Irak. Taarifa hiyo pia iliongeza kusema kwamba mashambulizi zaidi
yako njiani endapo Amerika na Uingereza hazitaondoa majeshi yake Irak.
Nae waziri mkuu wa Uingereza Tony Blair aliropoka kwamba Waislamu
ndio walioishambulia London. Matamshi yake yamezusha hofu kubwa kwa
waislamu nchini Uingereza ambao sasa wanaitaka serikali ya Blair kuwalinda
kutoka mashambulizi ya wakristo watakaoamua kulipiza kisasi. Walimlaumu
Brair na Bush wa Marekani kwa sera zao mbovu kuwahusu waislamu, ambazo
ndizo zinazochochea mashambulizi ya kila mara na maisha ya watu wasio
na hatia kupotea. Walimtaka Brair ajilaumu mwenyewe kabla hajaanza
kuwalaumu Waislamu. Walionya kwamba endapo Amerika na Uingereza hawataacha
kuwakandamiza Waislamu, basi mashambulizi kama haya hayatakoma duniani.
Wadadisi wa mambo wanasema kwamba Tangu Amerika iamue kuishambulia
Irak kwa kile ilichokiita kumaliza ughaidi duniani, mambo yamekuwa
kinyume chake. Badala ya ughaidi kumalizika, inaonekana kwamba hatua
ya Marekani imechangia kuongeza ughaidi badala ya kuupunguza. Kwamba
maghaidi wanaweza kuishambulia London asubuhi na kuharibu sekta ya
usafiri kabisa, hiyo inaonyesha kwamba maghaidi wanaweza kushambulia
popote na wakati wowote. Kwa sasa London wanajifariji kwamba walijua
itatokea. Swali wengi wanalouliza ni kwamba kama walijua, mbona hawakuzuia?




